logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Martha Karua azidua Chama kipya cha People Liberation Party (PLP)

Chama hicho kilizinduliwa kuchukua nafasi ya chama cha awali cha Narc Kenya chama ambacho kilikuwepo kwa miongo zaidi ya miwili.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri27 February 2025 - 16:00

Muhtasari


  • Chama hicho kilizinduliwa kuchukua nafasi ya chama cha awali cha Narc Kenya chama ambacho kilikuwepo kwa miongo zaidi ya miwili.
  • PLP ni chama ambacho kilizinduliwa kwa misingi ya Demokrasia,uwajibikaji na Usawa maelezo ya dibaji ya chama hicho yalieleza. Vilevile chama  hicho kilizinduliwa na kauanzisha uongozi wa mihula kwa kiongozi wa chama.


Aliyekuwa mgombea mwenza wa Azimio Martha Karua amezindua chama kipya cha People's Liberation Party (PLP)  katika makao makuu jijini Nairobi. 

Chama hicho kilizinduliwa kuchukua nafasi ya chama cha awali cha Narc Kenya chama ambacho kilikuwepo kwa miongo zaidi ya miwili.

PLP ni chama ambacho kilizinduliwa kwa misingi ya Demokrasia,uwajibikaji na Usawa maelezo ya dibaji ya chama hicho yalieleza. Vilevile chama  hicho kilizinduliwa na kauanzisha uongozi wa mihula kwa kiongozi wa chama.

Chama hicho kiliasisiwa kwa vigezo maalum vya kuendeleza uongozi ambao unaajibikia matakwa ya wananchi na kuipa kipaumbele  kauli ya chama ambayo ni Kuungana na kukomboana.

Baadhi ya wageni waliohudhuria mkutano huo wa uzinduzi wa chama hicho ni Kinara wa Wiper Daktari Stephine Musyoka,Eugine Wamalwa,Rigathi Gachagua,Morara Kebaso,Jimmy Wanjigi,Mukhisa Kituyi na Kivutha Kibwana.

Katika usemi wake Eugine Wamalwa aliwarai vijana wa kisasa wa Gen Z kuwaunga mkono ili wakomboe nchi  kutoka kwa utawala mbaya wa rais William Ruto akisema kuwa ukombozi huo utajumuisha vijana,kanisa na viongozi wote.

Kwa upande wake kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka alitoa pendekezo la kuirasimisha  tarehe 25 Juni kila mwaka kuwa kama siku ya Kitaifa kwa kumbukumbu za kuwakumbuka na kukumbuka   kazi waliotekeleza vijana wa Gen Z  kwa kuandamana na kupinga uongozi mbaya tena wa kidekteta.

Alimpongeza sana kinara wa PLP Martha Karua kwa kuzindua chama na kuanzisha nuru na mwanga katika ukombozi wa taifa.

Aliyekuwa Naibu wa rais Rigathi Gachagua alisema kuwa kutokana na wingi wa watu waliwarai wamtume nyumbani  mara moja Rais Ruto Pamoja na utawala wake wa kiimla.

Rigathi Gachagua alisema chini ya  muda wa miaka miwili serikali ya Kenya Kwanza  ilisambaratisha Hospitali,elimu na Uchumi.

Katika usemi wa Rigathi Gachagua alisema kuwa kule Kareni kwa Naibu wa Rais Kithure Kindiki kulikuwa na bomba la kuhifadhi  pesa ambalo lilikuwa limewekwa pale kwa minajili ya kuhonga watu ambao wanahudhuria mikutano.

Vilevile Gachagua alisema kuwa kule Ikulu kulikuwa na bomba la  kuhifadhia pesa aina ya dola kwa kuwalipa na kuwahonga viongozi mbalimbali,vilevile alisema kuwa kuna Memo au arifa ambayo ilioandikwa  itakayopelekwa katika baraza la Magavana ili mashamba ya majela yauziwe wawekezaji.

Kwa upande wake Martha Karua alisema kuwa serikali ilikuwa ikibomoa nyumba za walalahoi na kuwapa wandani wake,alimkanya  kiongozi wa taifa kuwacha kuwateka nyara wageni wa nchi za kigeni kwa kuungana na kuwateka nyara wananchi kutoka mataifa ya jumuiya ya Afrika Mashariki .

Aliwakumbusha kuwa mamlaka ya viongozi wa serikali yote  upo  kwa mwananchi mpiga kura  wala si kwa nguvu zao kama viongozi.  


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved